Google ni
ulimwengu wa uvumbuzi wa bidhaa na majaribio ya teknolojia, katika
baadhi ya mawazo na uvumbuzi ambao Google wanaendelea kufanyia kazi kuna
mambo ambayo sio ya kufikirika, gari inayojiendesha na kompyuta ya
kuvaa kama miwani ni miongoni mwa teknolojia hizo, kwa mtazamo wa haraka
unaweza kudhani kuwa itachukua miaka zaidi ya 10 Google kuweza kuziuza
bidhaa hizo kwa watu wa kawaida.
Ukweli
ni kwamba Google imeshatangaza kuwa Google Glass itaanza kuuzwa mwaka
huu wa 2013. Google Glass ni kompyuta ambayo huvaliwa kama miwani na ina
uwezo na matumizi mbali mbali kama vile kurekodi video na kupiga picha.
Katika ongezo jipya la Google Glass ni kwamba kompyuta hiyo itaweza
kutumia amri za sauti (voice command), kuanzisha amri ya sauti unatakiwa
kuiambia miwani hiyo “OK Glass” na miwani itaanza kukusikiliza unataka
ifanye nini kabla ya kuipa amri kama vile “record video”. Pia Google
wameonyesha baadhi ya matumizi ya miwani hiyo ambayo ni ya kawaida
kabisa mbali na yale ya kuchupa na parashuti kutoka kwenye ndege.
Matumizi hayo
ni pamoja na kurekodi video na kupiga picha wakati wa kuendesha gari,
unapocheza tenis na wakati wa kupanda mlima, pia Google imeonyesha
matumizi ya Miwani kwa wapanda pembea na wacheza muziki. Miwani hii
huenda ikatufanya Waswahili wengi zaidi kuamua kuupanda Mlima wa
Kilimanjaro. Pia Google glass itaweza kutoa taarifa kama vile urefu wa
barabara unayotembea, ni wakati gani ndege inatarajiwa kutua uwanjani,
kutafsiri maneno kutoka lugha moja kwenda nyingine na kukwambia
umesimama mtaa gani na hata kukuelekeza njia. Kwa kifupi Google
wanaelekea kuipa miwani hiyo uwezo wa “Google Now” ambayo ni search
engine inayotumia maneno.
Google
tayari imeanza kuwauzia miwani hiyo watengeneza apps (developers) ili
waweze kuanza kutengeza apps za miwani hii kwa matumizi mbali mbali.
Miwani hiyo itawagharimu developers jumla ya $1,500.00, kwa miwani moja
ambazo ni sawa na fedha taslimu za Kitanzania 2,451,000. Google pia
imethibitisha kuwa miwani hiyo itakuwa na Apps za simu na tablet za iOS
na Android ili kuweza kushirikiana na gajeti hizo katika utendaji wa
mambo mbali mbali kama vile ku-send message.
Ingawa
teknolojia hii ni mapema mno kujua itakuwa na uwezo na matumizi ya aina
gani hasa mbali na haya machache tuliyoyaeleza, wengi miongoni mwa
developers wanaelekewa kuvutiwa nayo kwa kiasi kikubwa. Google pia
imeanzisha mashindano kwa watu binafsi kuwaandikia twitter au Google+
kueleza ni jinsi gani miwani hii itatumika. Miongoni mwa masharti ya
shindano hilo ni kuwa maneno yasizidi 50, video isizidi sekunde 15,
picha zisizozidi 5 na utumie hashtag #ifihadglass. Kisha unatakiwa
ufuatilie Google+ (+ProjectGlass) au Twitter (@projectglass)
na Google imeahidi kujibu direct message kwa washindi. Zawadi kwa
washindi ni kuwa kupata nafasi ya kuinunua miwani hiyo mapema, hivyo
ukishinda uweke tayari T Sh. Milioni mbili na nusu.