Kushoto ni Zuckerberg Mwanasheria, kulia Zuckerberg “Toddler CEO” wa Facebook
Facebook ni neno ambalo kila mwenye kutumia kompyuta au simu zenye app ya Facebook hulisema karibu kila siku bila kujali lugha anayozungumza, hivi karibuni kampuni hiyo imefanya kituko cha kufuta akaunti ya Mark Zuckerberg. Mark Zuckerberg ni mmiliki na Afisa Mtendaji mkuu wa Facebook.

 Hata hivyo akaunti iliyofutwa si ya Zuckerberg anayemiliki Facebook. Sakata hilo lililotokea wiki hii limetokana na kuchanganyikiwa kwa wasimamizi wa Facebook kwa kudhani Mark S. Zuckerberg mwanasheria maarufu wa Indianapolis anaiga  jina la bosi wao. Facebook baadae wamegundua kosa lao hivyo kumuomba radhi mwanasheria huyo ambaye ni wakili anayetetea watu na makampuni yaliyofilisika. Facebook imo mbioni kuirejesha akaunti hiyo.
Zuckerberg mwanasheria si mshabiki sana wa Facebook, lakini ametumia tukio hili kujitangaza na kujiongezea umaarufu, Zuckerberg anatarajia kwamba umaarufu huo utamfungulia soko jipya na kupata wateja zaidi. Mwanasheria huyo amefungua website yenye anuani iammarkzuckerberg.com akiwaelezea watu kwamba naye ni mwenye jina hilo.
Zuckerberg huyu anadai yeye haipendi Faceook kwa vile imesababisha kuvunjika kwa ndoa yake lakini yupo humo kwa vile anatangaza biashara yake tu. Pia amedai kuwa Facebook imemsababishia matatizo mengi ikiwa ni pamoja na kusumbuliwa na watu wanaompigia simu wakiomba kutatuliwa matatizo ya Facebook au msaada wa kufanya mambo fulani mbali mbali katika mtandao huo. 
Zuckerberg mwanasheria anadai kwamba iwapo uli-gugul (google) Mark Zuckerberg katika miaka ya 2004 au kabla basi hakika ulinipata mimi, lakini sasa inabidi ugugul “Mark Zuckerberg Bankruptcy” kwa vile Zukerberg wa facebook ni maarufu zaidi. Kama tulivyoeleza awali mwanasheria huyu ametumia nafasi hii vizuri kwa kujitangaza.
SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO
 
Top