Sonara wa Liverpool, Uingereza Stuart Hughes ametengeneza iPhone 5 ya dhahabu na almasi halisi, yaani sio tu ya kuchovya. Kwa mujibu wa mtandao rasmi wa Stuart Hughes gamba zima la simu hiyo ni la dhahabu ya kareti 24 na logo ya Apple, kifungo cha mbele cha simu na mzunguko mzima wa simu umewekwa vipande vya almasi ya nyeusi ya kareti 26. iPhone hiyo unauzwa kwa jumla ya paundi za Uingereza milioni kumi sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 24.8
Sonara huyu ambaye hutengeneza gajeti, samani, mapambo ya gari, mapambo ya nyumba, mapambo ya boti na vifaa vyengine na kuvifanya viwe vya anasa na bei ya hali ya juu kwa ajili ya matajiri wa Dunia. Bila ya shaka yoyote kwa bei hii iPhone 5 hii ndio inakuwa simu ya ghali kuliko zote Duniani. Kwa mujibu wa maelezo ya Stuart Hughes imechukua jumla ya wiki tisa kuitengeneza simu hii. Simu hiyo imepewa jina la iPhone 5 Black Diamond yaani iPhone 5 ya almasi nyeusi.

Simu hiyo imebaki ikiwa na maumbile halisi la iPhone 5 ambapo kifungo cha nyumbani (home button) kimetengenezwa kwa almasi kiasi cha circa 600, ambazo zimelaziwa kwa maji ya dhahabu kabla ya kukauka kwake. Nembo ya Apple imewekewa jumla ya vipande vya alamasi 53. Jumla ya dhahabu iliyowekwa kwenye simu hiyo ina uzito wa gramu 153. Na aina ya almasi iliyotumika ni almasi nyeusi. 
Mbali na simu hii Stuart Hughes pia ametengeneza iPhone nyingine mbali mbali kwa dhahabu chache na bei nafuu mno kulinganisha na iPhone 5 Blakc Diamond. Kwa mfano iPhone 5 ya dhahabu ya kareti 24 ambayo imewekwa dhahabu  chache, yaani sehemu ya nyuma na mzunguko wa fremu ya simu inapatikana kwa Karibu £2695 sawa na shilingi milioni sita na laki saba, ambapo hii hata matajiri wa kwetu wataweza kununua kama wataamua kufanya hivyo.
SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO
 
Top