Wataalam
katika Chuo Kikuu cha Carlifonia wamo katika harakati za kutengeneza
chip ambayo itawekwa kwenye simu na kuwa na uwezo ya kugundua vijidudu
vya Malaria kwenye mwili wa binadamu. Wanasayansi wawili wa Chuo hicho
Peter Lilhoj na Chih-Ming Ho tayari wameshapata ruhusa ya kutengeneza
kifaa hicho kutoka kwenye vyombo husika. Kifaa hicho kitakuwa kinatumika
mara moja na kutupwa (disposable) na hivyo bila ya shaka kitakuwa ni
kifaa cha kuchomeka tu badala ya kutengenezwa ndani ya simu. Kitakuwa
kinafanana na kadi ya sim, kwa hiyo ni watumaini yetu kuwa kitatumika
kwenye nafasi ya kadi kwa maana ya kwamba hakutakuwa na simu maalum
yenye kufanya kazi hii, bali ni simu zote.
Wakati
wametuacha bado tukitafakari ni vipi simu itapima na kugundua kilichopo
kwenye damu, wataalam hao wameeleza kuwa lengo la mradi huu ni
kurahisisha na kusambaza upimaji na ugunduaji mapema wa maradhi haya
ambayo mpaka sasa yameshateketeza maisha wa watu wengi mno Duniani na
hasa katika nchi zilizoko Amerika ya Kusini, Afrika na Bara Hindi. Mradi
huu unategemea kuanza kutumika nchini Msumbiji katika maeneo ya
vijijini mara tu baada ya kukamilika kwa utengenezajiwa kifaa hichi.
Bila shaka hii italeta faraja kubwa katika kuigundua Malaria hata hivyo
matibabu hayatabadilika. Chuo Kikuu cha Carlifonia hakikuthibitisha ni
lini kifaa hichi kitakuwa tayari kutumika.