Wataalam katika Chuo Kikuu cha Carlifonia wamo katika harakati za kutengeneza chip ambayo itawekwa kwenye simu na kuwa na uwezo ya kugundua vijidudu vya Malaria kwenye mwili wa binadamu. Wanasayansi wawili wa Chuo hicho Peter Lilhoj na Chih-Ming Ho tayari wameshapata ruhusa ya kutengeneza kifaa hicho kutoka kwenye vyombo husika. Kifaa hicho kitakuwa kinatumika mara moja na kutupwa (disposable) na hivyo bila ya shaka kitakuwa ni kifaa cha kuchomeka tu badala ya kutengenezwa ndani ya simu. Kitakuwa kinafanana na kadi ya sim, kwa hiyo ni watumaini yetu kuwa kitatumika kwenye nafasi ya kadi kwa maana ya kwamba hakutakuwa na simu maalum yenye kufanya kazi hii, bali ni simu zote.


Wakati wametuacha bado tukitafakari ni vipi simu itapima na kugundua kilichopo kwenye damu, wataalam hao wameeleza kuwa lengo  la mradi huu ni kurahisisha na kusambaza upimaji na ugunduaji mapema wa maradhi haya ambayo mpaka sasa yameshateketeza maisha wa watu wengi mno Duniani na hasa katika nchi zilizoko Amerika ya Kusini, Afrika na Bara Hindi. Mradi huu unategemea kuanza kutumika nchini Msumbiji katika maeneo ya vijijini mara tu baada ya kukamilika kwa utengenezajiwa kifaa hichi. Bila shaka hii italeta faraja kubwa katika kuigundua Malaria hata hivyo matibabu hayatabadilika. Chuo Kikuu cha Carlifonia hakikuthibitisha ni lini kifaa hichi kitakuwa tayari kutumika.
SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO
 
Top