Kampuni ya Microsoft imeingia jikoni kuanza kupika software ambayo itatumiaka kwa njia ya mtandao (remote network) kuingizwa katika tableti au kompyuta. Huduma hiyo ambayo inatarajiwa kuwa ni sehemu ya Windows miaka ijayo imepewa jina la awali Microsoft Mohoro. Mohoro ni jina la mji uliopo kusini mashariki mwa kisiwa cha Ngazija (Comoro)  karibu na mji wa Fumbuni. 

Microsoft Mohoro bado ipo katika hatua za awali ambapo kwa mujibu wa taarifa za Business Insider, Mohoro itakuwa ndio njia mpya ya kutumia Windows ikiwa kama huduma ya desktop, hii ina maana kwamba itaweza kuwekwa kwenye kompyuta au tableti kwa njia ya mtandao kwa kutumia kompyuta nyingine, kupitia Mohoro tableti na kompyuta zitaweza kuwekewa Windows kwa njia ya beaming (kurushwa kwa kutumia internet) 

Katika hatua hizi za awali Microsoft bado hawakutoa taarifa rasmi ya huduma au software hii, ambapo kwa taarifa za CNet imeelezwa kwamba huduma hii itarajiwe kuwa tayari katikati ya mwaka 2014. Hii ina maana vifaa visivyotumia Windows kama vile iPad au tableti za Android huenda vitaweza kutumia OS hiyo katika mazingira ya virtual. 

Mohoro itakuwa ni jaribio la kwanza kabisa la Microsoft kufanya kitu cha namna hii, ila inaaminika kuwa Microsoft watatoa taarifa zaidi kuhusu Mohoro kwenye mkutano wa watengenezaji wa programu za Microsoft utakaofanyika mwezi wa Tisa mwaka huu. Bila shaka jamaa zangu kutoka Mohoro, Moroni hadi Mitsamiouli wataburudishwa na jina la programu hii. Ngarijo onana maudu. 
SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO
 
Top